Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

76 Al-'Insān ٱلْإِنْسَان

< Previous   31 Āyah   The Man      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

76:1 هَلْ أَتَىٰ عَلَى ٱلْإِنسَـٰنِ حِينٌ مِّنَ ٱلدَّهْرِ لَمْ يَكُن شَيْـًٔا مَّذْكُورًا
76:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.

76:2 إِنَّا خَلَقْنَا ٱلْإِنسَـٰنَ مِن نُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ نَّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَـٰهُ سَمِيعًۢا بَصِيرًا
76:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.

76:3 إِنَّا هَدَيْنَـٰهُ ٱلسَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا
76:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.

76:4 إِنَّآ أَعْتَدْنَا لِلْكَـٰفِرِينَ سَلَـٰسِلَا۟ وَأَغْلَـٰلًا وَسَعِيرًا
76:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.

76:5 إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ يَشْرَبُونَ مِن كَأْسٍ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا
76:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,

76:6 عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا عِبَادُ ٱللَّهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفْجِيرًا
76:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.

76:7 يُوفُونَ بِٱلنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُۥ مُسْتَطِيرًا
76:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,

76:8 وَيُطْعِمُونَ ٱلطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِۦ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا
76:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.

76:9 إِنَّمَا نُطْعِمُكُمْ لِوَجْهِ ٱللَّهِ لَا نُرِيدُ مِنكُمْ جَزَآءً وَلَا شُكُورًا
76:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.

76:10 إِنَّا نَخَافُ مِن رَّبِّنَا يَوْمًا عَبُوسًا قَمْطَرِيرًا
76:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.

76:11 فَوَقَىٰهُمُ ٱللَّهُ شَرَّ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمِ وَلَقَّىٰهُمْ نَضْرَةً وَسُرُورًا
76:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha na raha na furaha.

76:12 وَجَزَىٰهُم بِمَا صَبَرُوا۟ جَنَّةً وَحَرِيرًا
76:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.

76:13 مُّتَّكِـِٔينَ فِيهَا عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ ۖ لَا يَرَوْنَ فِيهَا شَمْسًا وَلَا زَمْهَرِيرًا
76:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.

76:14 وَدَانِيَةً عَلَيْهِمْ ظِلَـٰلُهَا وَذُلِّلَتْ قُطُوفُهَا تَذْلِيلًا
76:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.

76:15 وَيُطَافُ عَلَيْهِم بِـَٔانِيَةٍ مِّن فِضَّةٍ وَأَكْوَابٍ كَانَتْ قَوَارِيرَا۠
76:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,

76:16 قَوَارِيرَا۟ مِن فِضَّةٍ قَدَّرُوهَا تَقْدِيرًا
76:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.

76:17 وَيُسْقَوْنَ فِيهَا كَأْسًا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا
76:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.

76:18 عَيْنًا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلْسَبِيلًا
76:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.

76:19 ۞ وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيْتَهُمْ حَسِبْتَهُمْ لُؤْلُؤًا مَّنثُورًا
76:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.

76:20 وَإِذَا رَأَيْتَ ثَمَّ رَأَيْتَ نَعِيمًا وَمُلْكًا كَبِيرًا
76:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.

76:21 عَـٰلِيَهُمْ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضْرٌ وَإِسْتَبْرَقٌ ۖ وَحُلُّوٓا۟ أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٍ وَسَقَىٰهُمْ رَبُّهُمْ شَرَابًا طَهُورًا
76:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.

76:22 إِنَّ هَـٰذَا كَانَ لَكُمْ جَزَآءً وَكَانَ سَعْيُكُم مَّشْكُورًا
76:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.

76:23 إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا عَلَيْكَ ٱلْقُرْءَانَ تَنزِيلًا
76:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.

76:24 فَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تُطِعْ مِنْهُمْ ءَاثِمًا أَوْ كَفُورًا
76:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.

76:25 وَٱذْكُرِ ٱسْمَ رَبِّكَ بُكْرَةً وَأَصِيلًا
76:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;

76:26 وَمِنَ ٱلَّيْلِ فَٱسْجُدْ لَهُۥ وَسَبِّحْهُ لَيْلًا طَوِيلًا
76:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.

76:27 إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ يُحِبُّونَ ٱلْعَاجِلَةَ وَيَذَرُونَ وَرَآءَهُمْ يَوْمًا ثَقِيلًا
76:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.

76:28 نَّحْنُ خَلَقْنَـٰهُمْ وَشَدَدْنَآ أَسْرَهُمْ ۖ وَإِذَا شِئْنَا بَدَّلْنَآ أَمْثَـٰلَهُمْ تَبْدِيلًا
76:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.

76:29 إِنَّ هَـٰذِهِۦ تَذْكِرَةٌ ۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ سَبِيلًا
76:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.

76:30 وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ ۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمًا
76:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.

76:31 يُدْخِلُ مَن يَشَآءُ فِى رَحْمَتِهِۦ ۚ وَٱلظَّـٰلِمِينَ أَعَدَّ لَهُمْ عَذَابًا أَلِيمًۢا
76:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.