Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

44 Ad-Dukhān ٱلدُّخَان

< Previous   59 Āyah   The Smoke      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

44:1 حمٓ
44:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
H'a Mim

44:2 وَٱلْكِتَـٰبِ ٱلْمُبِينِ
44:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,

44:3 إِنَّآ أَنزَلْنَـٰهُ فِى لَيْلَةٍ مُّبَـٰرَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ
44:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.

44:4 فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ
44:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,

44:5 أَمْرًا مِّنْ عِندِنَآ ۚ إِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ
44:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.

44:6 رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ ۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ
44:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.

44:7 رَبِّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
44:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.

44:8 لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْىِۦ وَيُمِيتُ ۖ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
44:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.

44:9 بَلْ هُمْ فِى شَكٍّ يَلْعَبُونَ
44:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Lakini wao wanacheza katika shaka.

44:10 فَٱرْتَقِبْ يَوْمَ تَأْتِى ٱلسَّمَآءُ بِدُخَانٍ مُّبِينٍ
44:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,

44:11 يَغْشَى ٱلنَّاسَ ۖ هَـٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٌ
44:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!

44:12 رَّبَّنَا ٱكْشِفْ عَنَّا ٱلْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ
44:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.

44:13 أَنَّىٰ لَهُمُ ٱلذِّكْرَىٰ وَقَدْ جَآءَهُمْ رَسُولٌ مُّبِينٌ
44:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.

44:14 ثُمَّ تَوَلَّوْا۟ عَنْهُ وَقَالُوا۟ مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ
44:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.

44:15 إِنَّا كَاشِفُوا۟ ٱلْعَذَابِ قَلِيلًا ۚ إِنَّكُمْ عَآئِدُونَ
44:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!

44:16 يَوْمَ نَبْطِشُ ٱلْبَطْشَةَ ٱلْكُبْرَىٰٓ إِنَّا مُنتَقِمُونَ
44:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.

44:17 ۞ وَلَقَدْ فَتَنَّا قَبْلَهُمْ قَوْمَ فِرْعَوْنَ وَجَآءَهُمْ رَسُولٌ كَرِيمٌ
44:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.

44:18 أَنْ أَدُّوٓا۟ إِلَىَّ عِبَادَ ٱللَّهِ ۖ إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
44:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.

44:19 وَأَن لَّا تَعْلُوا۟ عَلَى ٱللَّهِ ۖ إِنِّىٓ ءَاتِيكُم بِسُلْطَـٰنٍ مُّبِينٍ
44:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.

44:20 وَإِنِّى عُذْتُ بِرَبِّى وَرَبِّكُمْ أَن تَرْجُمُونِ
44:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.

44:21 وَإِن لَّمْ تُؤْمِنُوا۟ لِى فَٱعْتَزِلُونِ
44:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.

44:22 فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ قَوْمٌ مُّجْرِمُونَ
44:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.

44:23 فَأَسْرِ بِعِبَادِى لَيْلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
44:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.

44:24 وَٱتْرُكِ ٱلْبَحْرَ رَهْوًا ۖ إِنَّهُمْ جُندٌ مُّغْرَقُونَ
44:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.

44:25 كَمْ تَرَكُوا۟ مِن جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
44:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!

44:26 وَزُرُوعٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ
44:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mimea na vyeo vitukufu!

44:27 وَنَعْمَةٍ كَانُوا۟ فِيهَا فَـٰكِهِينَ
44:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!

44:28 كَذَٰلِكَ ۖ وَأَوْرَثْنَـٰهَا قَوْمًا ءَاخَرِينَ
44:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.

44:29 فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ ٱلسَّمَآءُ وَٱلْأَرْضُ وَمَا كَانُوا۟ مُنظَرِينَ
44:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.

44:30 وَلَقَدْ نَجَّيْنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ مِنَ ٱلْعَذَابِ ٱلْمُهِينِ
44:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,

44:31 مِن فِرْعَوْنَ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيًا مِّنَ ٱلْمُسْرِفِينَ
44:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.

44:32 وَلَقَدِ ٱخْتَرْنَـٰهُمْ عَلَىٰ عِلْمٍ عَلَى ٱلْعَـٰلَمِينَ
44:32
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.

44:33 وَءَاتَيْنَـٰهُم مِّنَ ٱلْـَٔايَـٰتِ مَا فِيهِ بَلَـٰٓؤٌا۟ مُّبِينٌ
44:33
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.

44:34 إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ
44:34
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika hawa wanasema:

44:35 إِنْ هِىَ إِلَّا مَوْتَتُنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُنشَرِينَ
44:35
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.

44:36 فَأْتُوا۟ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ
44:36
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.

44:37 أَهُمْ خَيْرٌ أَمْ قَوْمُ تُبَّعٍ وَٱلَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ أَهْلَكْنَـٰهُمْ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ مُجْرِمِينَ
44:37
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.

44:38 وَمَا خَلَقْنَا ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَـٰعِبِينَ
44:38
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.

44:39 مَا خَلَقْنَـٰهُمَآ إِلَّا بِٱلْحَقِّ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ
44:39
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.

44:40 إِنَّ يَوْمَ ٱلْفَصْلِ مِيقَـٰتُهُمْ أَجْمَعِينَ
44:40
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.

44:41 يَوْمَ لَا يُغْنِى مَوْلًى عَن مَّوْلًى شَيْـًٔا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ
44:41
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.

44:42 إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُ ۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
44:42
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

44:43 إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ
44:43
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Mti wa Zaqqum,

44:44 طَعَامُ ٱلْأَثِيمِ
44:44
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ni chakula cha mwenye dhambi.

44:45 كَٱلْمُهْلِ يَغْلِى فِى ٱلْبُطُونِ
44:45
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni

44:46 كَغَلْىِ ٱلْحَمِيمِ
44:46
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kama kutokota kwa maji ya moto.

44:47 خُذُوهُ فَٱعْتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ
44:47
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!

44:48 ثُمَّ صُبُّوا۟ فَوْقَ رَأْسِهِۦ مِنْ عَذَابِ ٱلْحَمِيمِ
44:48
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.

44:49 ذُقْ إِنَّكَ أَنتَ ٱلْعَزِيزُ ٱلْكَرِيمُ
44:49
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!

44:50 إِنَّ هَـٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمْتَرُونَ
44:50
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.

44:51 إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى مَقَامٍ أَمِينٍ
44:51
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,

44:52 فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
44:52
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika mabustani na chemchem,

44:53 يَلْبَسُونَ مِن سُندُسٍ وَإِسْتَبْرَقٍ مُّتَقَـٰبِلِينَ
44:53
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,

44:54 كَذَٰلِكَ وَزَوَّجْنَـٰهُم بِحُورٍ عِينٍ
44:54
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.

44:55 يَدْعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَـٰكِهَةٍ ءَامِنِينَ
44:55
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.

44:56 لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلْمَوْتَ إِلَّا ٱلْمَوْتَةَ ٱلْأُولَىٰ ۖ وَوَقَىٰهُمْ عَذَابَ ٱلْجَحِيمِ
44:56
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,

44:57 فَضْلًا مِّن رَّبِّكَ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ
44:57
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

44:58 فَإِنَّمَا يَسَّرْنَـٰهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ
44:58
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.

44:59 فَٱرْتَقِبْ إِنَّهُم مُّرْتَقِبُونَ
44:59
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ngoja tu, na wao wangoje pia.