Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

15 Al-Ĥijr ٱلْحِجْر

< Previous   99 Āyah   The Rocky Tract      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

15:1 الٓر ۚ تِلْكَ ءَايَـٰتُ ٱلْكِتَـٰبِ وَقُرْءَانٍ مُّبِينٍ
15:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.

15:2 رُّبَمَا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لَوْ كَانُوا۟ مُسْلِمِينَ
15:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.

15:3 ذَرْهُمْ يَأْكُلُوا۟ وَيَتَمَتَّعُوا۟ وَيُلْهِهِمُ ٱلْأَمَلُ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
15:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.

15:4 وَمَآ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا وَلَهَا كِتَابٌ مَّعْلُومٌ
15:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.

15:5 مَّا تَسْبِقُ مِنْ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسْتَـْٔخِرُونَ
15:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.

15:6 وَقَالُوا۟ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِى نُزِّلَ عَلَيْهِ ٱلذِّكْرُ إِنَّكَ لَمَجْنُونٌ
15:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.

15:7 لَّوْ مَا تَأْتِينَا بِٱلْمَلَـٰٓئِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
15:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?

15:8 مَا نُنَزِّلُ ٱلْمَلَـٰٓئِكَةَ إِلَّا بِٱلْحَقِّ وَمَا كَانُوٓا۟ إِذًا مُّنظَرِينَ
15:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.

15:9 إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا ٱلذِّكْرَ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَـٰفِظُونَ
15:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.

15:10 وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ فِى شِيَعِ ٱلْأَوَّلِينَ
15:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.

15:11 وَمَا يَأْتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ
15:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.

15:12 كَذَٰلِكَ نَسْلُكُهُۥ فِى قُلُوبِ ٱلْمُجْرِمِينَ
15:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.

15:13 لَا يُؤْمِنُونَ بِهِۦ ۖ وَقَدْ خَلَتْ سُنَّةُ ٱلْأَوَّلِينَ
15:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.

15:14 وَلَوْ فَتَحْنَا عَلَيْهِم بَابًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ فَظَلُّوا۟ فِيهِ يَعْرُجُونَ
15:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,

15:15 لَقَالُوٓا۟ إِنَّمَا سُكِّرَتْ أَبْصَـٰرُنَا بَلْ نَحْنُ قَوْمٌ مَّسْحُورُونَ
15:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.

15:16 وَلَقَدْ جَعَلْنَا فِى ٱلسَّمَآءِ بُرُوجًا وَزَيَّنَّـٰهَا لِلنَّـٰظِرِينَ
15:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.

15:17 وَحَفِظْنَـٰهَا مِن كُلِّ شَيْطَـٰنٍ رَّجِيمٍ
15:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.

15:18 إِلَّا مَنِ ٱسْتَرَقَ ٱلسَّمْعَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌ مُّبِينٌ
15:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.

15:19 وَٱلْأَرْضَ مَدَدْنَـٰهَا وَأَلْقَيْنَا فِيهَا رَوَٰسِىَ وَأَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ شَىْءٍ مَّوْزُونٍ
15:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.

15:20 وَجَعَلْنَا لَكُمْ فِيهَا مَعَـٰيِشَ وَمَن لَّسْتُمْ لَهُۥ بِرَٰزِقِينَ
15:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.

15:21 وَإِن مِّن شَىْءٍ إِلَّا عِندَنَا خَزَآئِنُهُۥ وَمَا نُنَزِّلُهُۥٓ إِلَّا بِقَدَرٍ مَّعْلُومٍ
15:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.

15:22 وَأَرْسَلْنَا ٱلرِّيَـٰحَ لَوَٰقِحَ فَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءً فَأَسْقَيْنَـٰكُمُوهُ وَمَآ أَنتُمْ لَهُۥ بِخَـٰزِنِينَ
15:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.

15:23 وَإِنَّا لَنَحْنُ نُحْىِۦ وَنُمِيتُ وَنَحْنُ ٱلْوَٰرِثُونَ
15:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.

15:24 وَلَقَدْ عَلِمْنَا ٱلْمُسْتَقْدِمِينَ مِنكُمْ وَلَقَدْ عَلِمْنَا ٱلْمُسْتَـْٔخِرِينَ
15:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.

15:25 وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحْشُرُهُمْ ۚ إِنَّهُۥ حَكِيمٌ عَلِيمٌ
15:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.

15:26 وَلَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَـٰنَ مِن صَلْصَـٰلٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
15:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.

15:27 وَٱلْجَآنَّ خَلَقْنَـٰهُ مِن قَبْلُ مِن نَّارِ ٱلسَّمُومِ
15:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.

15:28 وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَـٰٓئِكَةِ إِنِّى خَـٰلِقٌۢ بَشَرًا مِّن صَلْصَـٰلٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
15:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.

15:29 فَإِذَا سَوَّيْتُهُۥ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِن رُّوحِى فَقَعُوا۟ لَهُۥ سَـٰجِدِينَ
15:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.

15:30 فَسَجَدَ ٱلْمَلَـٰٓئِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَ
15:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,

15:31 إِلَّآ إِبْلِيسَ أَبَىٰٓ أَن يَكُونَ مَعَ ٱلسَّـٰجِدِينَ
15:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.

15:32 قَالَ يَـٰٓإِبْلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ ٱلسَّـٰجِدِينَ
15:32
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?

15:33 قَالَ لَمْ أَكُن لِّأَسْجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقْتَهُۥ مِن صَلْصَـٰلٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
15:33
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.

15:34 قَالَ فَٱخْرُجْ مِنْهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٌ
15:34
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!

15:35 وَإِنَّ عَلَيْكَ ٱللَّعْنَةَ إِلَىٰ يَوْمِ ٱلدِّينِ
15:35
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.

15:36 قَالَ رَبِّ فَأَنظِرْنِىٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
15:36
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.

15:37 قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلْمُنظَرِينَ
15:37
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula

15:38 إِلَىٰ يَوْمِ ٱلْوَقْتِ ٱلْمَعْلُومِ
15:38
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mpaka siku ya wakati maalumu.

15:39 قَالَ رَبِّ بِمَآ أَغْوَيْتَنِى لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمْ فِى ٱلْأَرْضِ وَلَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ
15:39
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,

15:40 إِلَّا عِبَادَكَ مِنْهُمُ ٱلْمُخْلَصِينَ
15:40
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ila waja wako walio safika.

15:41 قَالَ هَـٰذَا صِرَٰطٌ عَلَىَّ مُسْتَقِيمٌ
15:41
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.

15:42 إِنَّ عِبَادِى لَيْسَ لَكَ عَلَيْهِمْ سُلْطَـٰنٌ إِلَّا مَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلْغَاوِينَ
15:42
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.

15:43 وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوْعِدُهُمْ أَجْمَعِينَ
15:43
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.

15:44 لَهَا سَبْعَةُ أَبْوَٰبٍ لِّكُلِّ بَابٍ مِّنْهُمْ جُزْءٌ مَّقْسُومٌ
15:44
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.

15:45 إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
15:45
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.

15:46 ٱدْخُلُوهَا بِسَلَـٰمٍ ءَامِنِينَ
15:46
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.

15:47 وَنَزَعْنَا مَا فِى صُدُورِهِم مِّنْ غِلٍّ إِخْوَٰنًا عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَـٰبِلِينَ
15:47
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.

15:48 لَا يَمَسُّهُمْ فِيهَا نَصَبٌ وَمَا هُم مِّنْهَا بِمُخْرَجِينَ
15:48
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.

15:49 ۞ نَبِّئْ عِبَادِىٓ أَنِّىٓ أَنَا ٱلْغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ
15:49
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.

15:50 وَأَنَّ عَذَابِى هُوَ ٱلْعَذَابُ ٱلْأَلِيمُ
15:50
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!

15:51 وَنَبِّئْهُمْ عَن ضَيْفِ إِبْرَٰهِيمَ
15:51
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.

15:52 إِذْ دَخَلُوا۟ عَلَيْهِ فَقَالُوا۟ سَلَـٰمًا قَالَ إِنَّا مِنكُمْ وَجِلُونَ
15:52
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.

15:53 قَالُوا۟ لَا تَوْجَلْ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَـٰمٍ عَلِيمٍ
15:53
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.

15:54 قَالَ أَبَشَّرْتُمُونِى عَلَىٰٓ أَن مَّسَّنِىَ ٱلْكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ
15:54
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?

15:55 قَالُوا۟ بَشَّرْنَـٰكَ بِٱلْحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ ٱلْقَـٰنِطِينَ
15:55
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.

15:56 قَالَ وَمَن يَقْنَطُ مِن رَّحْمَةِ رَبِّهِۦٓ إِلَّا ٱلضَّآلُّونَ
15:56
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?

15:57 قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا ٱلْمُرْسَلُونَ
15:57
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?

15:58 قَالُوٓا۟ إِنَّآ أُرْسِلْنَآ إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
15:58
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!

15:59 إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمْ أَجْمَعِينَ
15:59
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.

15:60 إِلَّا ٱمْرَأَتَهُۥ قَدَّرْنَآ ۙ إِنَّهَا لَمِنَ ٱلْغَـٰبِرِينَ
15:60
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.

15:61 فَلَمَّا جَآءَ ءَالَ لُوطٍ ٱلْمُرْسَلُونَ
15:61
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,

15:62 قَالَ إِنَّكُمْ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
15:62
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.

15:63 قَالُوا۟ بَلْ جِئْنَـٰكَ بِمَا كَانُوا۟ فِيهِ يَمْتَرُونَ
15:63
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.

15:64 وَأَتَيْنَـٰكَ بِٱلْحَقِّ وَإِنَّا لَصَـٰدِقُونَ
15:64
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.

15:65 فَأَسْرِ بِأَهْلِكَ بِقِطْعٍ مِّنَ ٱلَّيْلِ وَٱتَّبِعْ أَدْبَـٰرَهُمْ وَلَا يَلْتَفِتْ مِنكُمْ أَحَدٌ وَٱمْضُوا۟ حَيْثُ تُؤْمَرُونَ
15:65
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.

15:66 وَقَضَيْنَآ إِلَيْهِ ذَٰلِكَ ٱلْأَمْرَ أَنَّ دَابِرَ هَـٰٓؤُلَآءِ مَقْطُوعٌ مُّصْبِحِينَ
15:66
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.

15:67 وَجَآءَ أَهْلُ ٱلْمَدِينَةِ يَسْتَبْشِرُونَ
15:67
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.

15:68 قَالَ إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ ضَيْفِى فَلَا تَفْضَحُونِ
15:68
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.

15:69 وَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَلَا تُخْزُونِ
15:69
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.

15:70 قَالُوٓا۟ أَوَلَمْ نَنْهَكَ عَنِ ٱلْعَـٰلَمِينَ
15:70
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?

15:71 قَالَ هَـٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِىٓ إِن كُنتُمْ فَـٰعِلِينَ
15:71
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.

15:72 لَعَمْرُكَ إِنَّهُمْ لَفِى سَكْرَتِهِمْ يَعْمَهُونَ
15:72
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.

15:73 فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّيْحَةُ مُشْرِقِينَ
15:73
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.

15:74 فَجَعَلْنَا عَـٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن سِجِّيلٍ
15:74
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.

15:75 إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَـٰتٍ لِّلْمُتَوَسِّمِينَ
15:75
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.

15:76 وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٍ مُّقِيمٍ
15:76
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.

15:77 إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً لِّلْمُؤْمِنِينَ
15:77
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.

15:78 وَإِن كَانَ أَصْحَـٰبُ ٱلْأَيْكَةِ لَظَـٰلِمِينَ
15:78
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.

15:79 فَٱنتَقَمْنَا مِنْهُمْ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٍ مُّبِينٍ
15:79
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.

15:80 وَلَقَدْ كَذَّبَ أَصْحَـٰبُ ٱلْحِجْرِ ٱلْمُرْسَلِينَ
15:80
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.

15:81 وَءَاتَيْنَـٰهُمْ ءَايَـٰتِنَا فَكَانُوا۟ عَنْهَا مُعْرِضِينَ
15:81
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.

15:82 وَكَانُوا۟ يَنْحِتُونَ مِنَ ٱلْجِبَالِ بُيُوتًا ءَامِنِينَ
15:82
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.

15:83 فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّيْحَةُ مُصْبِحِينَ
15:83
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.

15:84 فَمَآ أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ
15:84
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.

15:85 وَمَا خَلَقْنَا ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَآ إِلَّا بِٱلْحَقِّ ۗ وَإِنَّ ٱلسَّاعَةَ لَـَٔاتِيَةٌ ۖ فَٱصْفَحِ ٱلصَّفْحَ ٱلْجَمِيلَ
15:85
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.

15:86 إِنَّ رَبَّكَ هُوَ ٱلْخَلَّـٰقُ ٱلْعَلِيمُ
15:86
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.

15:87 وَلَقَدْ ءَاتَيْنَـٰكَ سَبْعًا مِّنَ ٱلْمَثَانِى وَٱلْقُرْءَانَ ٱلْعَظِيمَ
15:87
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.

15:88 لَا تَمُدَّنَّ عَيْنَيْكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعْنَا بِهِۦٓ أَزْوَٰجًا مِّنْهُمْ وَلَا تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ وَٱخْفِضْ جَنَاحَكَ لِلْمُؤْمِنِينَ
15:88
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.

15:89 وَقُلْ إِنِّىٓ أَنَا ٱلنَّذِيرُ ٱلْمُبِينُ
15:89
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.

15:90 كَمَآ أَنزَلْنَا عَلَى ٱلْمُقْتَسِمِينَ
15:90
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,

15:91 ٱلَّذِينَ جَعَلُوا۟ ٱلْقُرْءَانَ عِضِينَ
15:91
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.

15:92 فَوَرَبِّكَ لَنَسْـَٔلَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ
15:92
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,

15:93 عَمَّا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ
15:93
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

15:94 فَٱصْدَعْ بِمَا تُؤْمَرُ وَأَعْرِضْ عَنِ ٱلْمُشْرِكِينَ
15:94
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.

15:95 إِنَّا كَفَيْنَـٰكَ ٱلْمُسْتَهْزِءِينَ
15:95
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.

15:96 ٱلَّذِينَ يَجْعَلُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَـٰهًا ءَاخَرَ ۚ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
15:96
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!

15:97 وَلَقَدْ نَعْلَمُ أَنَّكَ يَضِيقُ صَدْرُكَ بِمَا يَقُولُونَ
15:97
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.

15:98 فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَكُن مِّنَ ٱلسَّـٰجِدِينَ
15:98
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.

15:99 وَٱعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأْتِيَكَ ٱلْيَقِينُ
15:99
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.