Selected
Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani
Abdullah Yusuf Ali
Abdul Majid Daryabadi
Abul Ala Maududi
Ahmed Ali
Ahmed Raza Khan
A. J. Arberry
Ali Quli Qarai
Hasan al-Fatih Qaribullah and Ahmad Darwish
Mohammad Habib Shakir
Mohammed Marmaduke William Pickthall
Muhammad Sarwar
Muhammad Taqi-ud-Din al-Hilali and Muhammad Muhsin Khan
Safi-ur-Rahman al-Mubarakpuri
Saheeh International
Talal Itani
Transliteration
Wahiduddin Khan
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.
26:1
طسٓمٓ
26:1
T'aa Siin Miim. (T'. S. M.) - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:2
تِلْكَ ءَايَـٰتُ ٱلْكِتَـٰبِ ٱلْمُبِينِ
26:2
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:3
لَعَلَّكَ بَـٰخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
26:3
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:4
إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةً فَظَلَّتْ أَعْنَـٰقُهُمْ لَهَا خَـٰضِعِينَ
26:4
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:5
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ ٱلرَّحْمَـٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا۟ عَنْهُ مُعْرِضِينَ
26:5
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:6
فَقَدْ كَذَّبُوا۟ فَسَيَأْتِيهِمْ أَنۢبَـٰٓؤُا۟ مَا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ
26:6
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:7
أَوَلَمْ يَرَوْا۟ إِلَى ٱلْأَرْضِ كَمْ أَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ
26:7
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:8
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:8
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:9
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:9
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:10
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئْتِ ٱلْقَوْمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ
26:10
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:11
قَوْمَ فِرْعَوْنَ ۚ أَلَا يَتَّقُونَ
26:11
Watu wa Firauni. Hawaogopi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:12
قَالَ رَبِّ إِنِّىٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
26:12
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:13
وَيَضِيقُ صَدْرِى وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِى فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَـٰرُونَ
26:13
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:14
وَلَهُمْ عَلَىَّ ذَنۢبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ
26:14
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:15
قَالَ كَلَّا ۖ فَٱذْهَبَا بِـَٔايَـٰتِنَآ ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ
26:15
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:16
فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:16
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:17
أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
26:17
Waachilie Wana wa Israili wende nasi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:18
قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ
26:18
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:19
وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ ٱلَّتِى فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلْكَـٰفِرِينَ
26:19
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:20
قَالَ فَعَلْتُهَآ إِذًا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
26:20
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:21
فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِى رَبِّى حُكْمًا وَجَعَلَنِى مِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:21
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:22
وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَىَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
26:22
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:23
قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:23
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:24
قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
26:24
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:25
قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُۥٓ أَلَا تَسْتَمِعُونَ
26:25
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:26
قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
26:26
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:27
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِىٓ أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ
26:27
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:28
قَالَ رَبُّ ٱلْمَشْرِقِ وَٱلْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ
26:28
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:29
قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذْتَ إِلَـٰهًا غَيْرِى لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ ٱلْمَسْجُونِينَ
26:29
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:30
قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَىْءٍ مُّبِينٍ
26:30
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:31
قَالَ فَأْتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
26:31
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:32
فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ
26:32
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:33
وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِىَ بَيْضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ
26:33
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:34
قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُۥٓ إِنَّ هَـٰذَا لَسَـٰحِرٌ عَلِيمٌ
26:34
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:35
يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِۦ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ
26:35
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:36
قَالُوٓا۟ أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَٱبْعَثْ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَـٰشِرِينَ
26:36
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:37
يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍ
26:37
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:38
فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَـٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
26:38
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:39
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ
26:39
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:40
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
26:40
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:41
فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُوا۟ لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
26:41
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:42
قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ
26:42
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:43
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلْقُوا۟ مَآ أَنتُم مُّلْقُونَ
26:43
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:44
فَأَلْقَوْا۟ حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا۟ بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ ٱلْغَـٰلِبُونَ
26:44
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:45
فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ
26:45
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:46
فَأُلْقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سَـٰجِدِينَ
26:46
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:47
قَالُوٓا۟ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:47
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:48
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
26:48
Mola Mlezi wa Musa na Harun. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:49
قَالَ ءَامَنتُمْ لَهُۥ قَبْلَ أَنْ ءَاذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِى عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَـٰفٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ
26:49
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:50
قَالُوا۟ لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
26:50
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:51
إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَـٰيَـٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:51
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:52
۞ وَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِىٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
26:52
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:53
فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَـٰشِرِينَ
26:53
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:54
إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ
26:54
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:55
وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَآئِظُونَ
26:55
Nao wanatuudhi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:56
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَـٰذِرُونَ
26:56
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:57
فَأَخْرَجْنَـٰهُم مِّن جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
26:57
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:58
وَكُنُوزٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ
26:58
Na makhazina, na vyeo vya hishima, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:59
كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَـٰهَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
26:59
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:60
فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ
26:60
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:61
فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَـٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ
26:61
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:62
قَالَ كَلَّآ ۖ إِنَّ مَعِىَ رَبِّى سَيَهْدِينِ
26:62
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:63
فَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضْرِب بِّعَصَاكَ ٱلْبَحْرَ ۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَٱلطَّوْدِ ٱلْعَظِيمِ
26:63
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:64
وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ ٱلْـَٔاخَرِينَ
26:64
Na tukawajongeza hapo wale wengine. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:65
وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
26:65
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:66
ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
26:66
Kisha tukawazamisha hao wengine. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:67
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:67
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:68
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:68
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:69
وَٱتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَٰهِيمَ
26:69
Na wasomee khabari za Ibrahim. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:70
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَا تَعْبُدُونَ
26:70
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:71
قَالُوا۟ نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَـٰكِفِينَ
26:71
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:72
قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ
26:72
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:73
أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ
26:73
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:74
قَالُوا۟ بَلْ وَجَدْنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ
26:74
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:75
قَالَ أَفَرَءَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
26:75
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu- - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:76
أَنتُمْ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلْأَقْدَمُونَ
26:76
Nyinyi na baba zenu wa zamani? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:77
فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّىٓ إِلَّا رَبَّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:77
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:78
ٱلَّذِى خَلَقَنِى فَهُوَ يَهْدِينِ
26:78
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:79
وَٱلَّذِى هُوَ يُطْعِمُنِى وَيَسْقِينِ
26:79
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:80
وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ
26:80
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:81
وَٱلَّذِى يُمِيتُنِى ثُمَّ يُحْيِينِ
26:81
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:82
وَٱلَّذِىٓ أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِى خَطِيٓـَٔتِى يَوْمَ ٱلدِّينِ
26:82
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:83
رَبِّ هَبْ لِى حُكْمًا وَأَلْحِقْنِى بِٱلصَّـٰلِحِينَ
26:83
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:84
وَٱجْعَل لِّى لِسَانَ صِدْقٍ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
26:84
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:85
وَٱجْعَلْنِى مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ
26:85
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:86
وَٱغْفِرْ لِأَبِىٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
26:86
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:87
وَلَا تُخْزِنِى يَوْمَ يُبْعَثُونَ
26:87
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:88
يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ
26:88
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:89
إِلَّا مَنْ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
26:89
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:90
وَأُزْلِفَتِ ٱلْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ
26:90
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:91
وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ
26:91
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:92
وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
26:92
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:93
مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ
26:93
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:94
فَكُبْكِبُوا۟ فِيهَا هُمْ وَٱلْغَاوُۥنَ
26:94
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:95
وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ
26:95
Na majeshi ya Ibilisi yote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:96
قَالُوا۟ وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ
26:96
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo: - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:97
تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِى ضَلَـٰلٍ مُّبِينٍ
26:97
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:98
إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:98
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:99
وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلْمُجْرِمُونَ
26:99
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:100
فَمَا لَنَا مِن شَـٰفِعِينَ
26:100
Basi hatuna waombezi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:101
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ
26:101
Wala rafiki wa dhati. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:102
فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:102
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:103
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:103
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:104
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:104
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:105
كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:105
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:106
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:106
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:107
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:107
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:108
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:108
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:109
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:109
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:110
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:110
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:111
۞ قَالُوٓا۟ أَنُؤْمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلْأَرْذَلُونَ
26:111
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:112
قَالَ وَمَا عِلْمِى بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ
26:112
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:113
إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّى ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ
26:113
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:114
وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:114
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:115
إِنْ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
26:115
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:116
قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَـٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمَرْجُومِينَ
26:116
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:117
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِى كَذَّبُونِ
26:117
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:118
فَٱفْتَحْ بَيْنِى وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِى وَمَن مَّعِىَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:118
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:119
فَأَنجَيْنَـٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
26:119
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:120
ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ ٱلْبَاقِينَ
26:120
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:121
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:121
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:122
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:122
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:123
كَذَّبَتْ عَادٌ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:123
Kina A'd waliwakanusha Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:124
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:124
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:125
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:125
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:126
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:126
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:127
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:127
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:128
أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةً تَعْبَثُونَ
26:128
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:129
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ
26:129
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:130
وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ
26:130
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:131
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:131
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:132
وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِىٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ
26:132
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:133
أَمَدَّكُم بِأَنْعَـٰمٍ وَبَنِينَ
26:133
Amekupeni wanyama wa kufuga na wana. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:134
وَجَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
26:134
Na mabustani na chemchem. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:135
إِنِّىٓ أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
26:135
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:136
قَالُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْنَآ أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ ٱلْوَٰعِظِينَ
26:136
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:137
إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلْأَوَّلِينَ
26:137
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:138
وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
26:138
Wala sisi hatutaadhibiwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:139
فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَـٰهُمْ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:139
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:140
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:140
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:141
كَذَّبَتْ ثَمُودُ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:141
Kina Thamud waliwakanusha Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:142
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَـٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:142
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:143
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:143
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:144
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:144
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:145
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:145
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:146
أَتُتْرَكُونَ فِى مَا هَـٰهُنَآ ءَامِنِينَ
26:146
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:147
فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
26:147
Katika mabustani, na chemchem? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:148
وَزُرُوعٍ وَنَخْلٍ طَلْعُهَا هَضِيمٌ
26:148
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:149
وَتَنْحِتُونَ مِنَ ٱلْجِبَالِ بُيُوتًا فَـٰرِهِينَ
26:149
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:150
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:150
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:151
وَلَا تُطِيعُوٓا۟ أَمْرَ ٱلْمُسْرِفِينَ
26:151
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:152
ٱلَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِى ٱلْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ
26:152
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:153
قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ
26:153
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:154
مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
26:154
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:155
قَالَ هَـٰذِهِۦ نَاقَةٌ لَّهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
26:155
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:156
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ
26:156
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:157
فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا۟ نَـٰدِمِينَ
26:157
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:158
فَأَخَذَهُمُ ٱلْعَذَابُ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:158
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:159
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:159
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:160
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:160
Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:161
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:161
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:162
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:162
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:163
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:163
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:164
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:164
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:165
أَتَأْتُونَ ٱلذُّكْرَانَ مِنَ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:165
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:166
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَٰجِكُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ
26:166
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:167
قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَـٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمُخْرَجِينَ
26:167
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:168
قَالَ إِنِّى لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلْقَالِينَ
26:168
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:169
رَبِّ نَجِّنِى وَأَهْلِى مِمَّا يَعْمَلُونَ
26:169
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:170
فَنَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
26:170
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:171
إِلَّا عَجُوزًا فِى ٱلْغَـٰبِرِينَ
26:171
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:172
ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
26:172
Kisha tukawaangamiza wale wengine. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:173
وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا ۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلْمُنذَرِينَ
26:173
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:174
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:174
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:175
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:175
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:176
كَذَّبَ أَصْحَـٰبُ لْـَٔيْكَةِ ٱلْمُرْسَلِينَ
26:176
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:177
إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
26:177
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:178
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
26:178
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:179
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
26:179
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:180
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:180
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:181
۞ أَوْفُوا۟ ٱلْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا۟ مِنَ ٱلْمُخْسِرِينَ
26:181
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:182
وَزِنُوا۟ بِٱلْقِسْطَاسِ ٱلْمُسْتَقِيمِ
26:182
Na pimeni kwa haki iliyo nyooka; - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:183
وَلَا تَبْخَسُوا۟ ٱلنَّاسَ أَشْيَآءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا۟ فِى ٱلْأَرْضِ مُفْسِدِينَ
26:183
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:184
وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِى خَلَقَكُمْ وَٱلْجِبِلَّةَ ٱلْأَوَّلِينَ
26:184
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:185
قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ
26:185
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:186
وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلْكَـٰذِبِينَ
26:186
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:187
فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ
26:187
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:188
قَالَ رَبِّىٓ أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ
26:188
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:189
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ ٱلظُّلَّةِ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
26:189
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:190
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
26:190
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:191
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
26:191
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:192
وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
26:192
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:193
نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلْأَمِينُ
26:193
Ameuteremsha Roho muaminifu, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:194
عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلْمُنذِرِينَ
26:194
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:195
بِلِسَانٍ عَرَبِىٍّ مُّبِينٍ
26:195
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:196
وَإِنَّهُۥ لَفِى زُبُرِ ٱلْأَوَّلِينَ
26:196
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:197
أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ ءَايَةً أَن يَعْلَمَهُۥ عُلَمَـٰٓؤُا۟ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
26:197
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:198
وَلَوْ نَزَّلْنَـٰهُ عَلَىٰ بَعْضِ ٱلْأَعْجَمِينَ
26:198
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:199
فَقَرَأَهُۥ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا۟ بِهِۦ مُؤْمِنِينَ
26:199
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:200
كَذَٰلِكَ سَلَكْنَـٰهُ فِى قُلُوبِ ٱلْمُجْرِمِينَ
26:200
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:201
لَا يُؤْمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُا۟ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ
26:201
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:202
فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ
26:202
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:203
فَيَقُولُوا۟ هَلْ نَحْنُ مُنظَرُونَ
26:203
Na watasema: Je, tutapewa muhula? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:204
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
26:204
Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:205
أَفَرَءَيْتَ إِن مَّتَّعْنَـٰهُمْ سِنِينَ
26:205
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:206
ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُوا۟ يُوعَدُونَ
26:206
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:207
مَآ أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا۟ يُمَتَّعُونَ
26:207
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:208
وَمَآ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
26:208
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji - - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:209
ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَـٰلِمِينَ
26:209
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:210
وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ ٱلشَّيَـٰطِينُ
26:210
Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:211
وَمَا يَنۢبَغِى لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ
26:211
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:212
إِنَّهُمْ عَنِ ٱلسَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ
26:212
Hakika hao wametengwa na kusikia. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:213
فَلَا تَدْعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَـٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلْمُعَذَّبِينَ
26:213
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:214
وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ ٱلْأَقْرَبِينَ
26:214
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:215
وَٱخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
26:215
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:216
فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّى بَرِىٓءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ
26:216
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:217
وَتَوَكَّلْ عَلَى ٱلْعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ
26:217
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:218
ٱلَّذِى يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ
26:218
Ambaye anakuona unapo simama, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:219
وَتَقَلُّبَكَ فِى ٱلسَّـٰجِدِينَ
26:219
Na mageuko yako kati ya wanao sujudu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:220
إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ
26:220
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:221
هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَـٰطِينُ
26:221
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:222
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ
26:222
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:223
يُلْقُونَ ٱلسَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَـٰذِبُونَ
26:223
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:224
وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلْغَاوُۥنَ
26:224
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:225
أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِى كُلِّ وَادٍ يَهِيمُونَ
26:225
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:226
وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ
26:226
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
26:227
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ وَذَكَرُوا۟ ٱللَّهَ كَثِيرًا وَٱنتَصَرُوا۟ مِنۢ بَعْدِ مَا ظُلِمُوا۟ ۗ وَسَيَعْلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓا۟ أَىَّ مُنقَلَبٍ يَنقَلِبُونَ
26:227
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)