Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

85 Al-Burūj ٱلْبُرُوج

< Previous   22 Āyah   The Mansions of the Stars      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

85:1 وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ
85:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Naapa kwa mbingu yenye Buruji!

85:2 وَٱلْيَوْمِ ٱلْمَوْعُودِ
85:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa siku iliyo ahidiwa!

85:3 وَشَاهِدٍ وَمَشْهُودٍ
85:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!

85:4 قُتِلَ أَصْحَـٰبُ ٱلْأُخْدُودِ
85:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wameangamizwa watu wa makhandaki

85:5 ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلْوَقُودِ
85:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Yenye moto wenye kuni nyingi,

85:6 إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌ
85:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Walipo kuwa wamekaa hapo,

85:7 وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِٱلْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌ
85:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.

85:8 وَمَا نَقَمُوا۟ مِنْهُمْ إِلَّآ أَن يُؤْمِنُوا۟ بِٱللَّهِ ٱلْعَزِيزِ ٱلْحَمِيدِ
85:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,

85:9 ٱلَّذِى لَهُۥ مُلْكُ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَىْءٍ شَهِيدٌ
85:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.

85:10 إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُوا۟ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَـٰتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا۟ فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ ٱلْحَرِيقِ
85:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.

85:11 إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ لَهُمْ جَنَّـٰتٌ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَـٰرُ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْفَوْزُ ٱلْكَبِيرُ
85:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

85:12 إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
85:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.

85:13 إِنَّهُۥ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ
85:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,

85:14 وَهُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلْوَدُودُ
85:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,

85:15 ذُو ٱلْعَرْشِ ٱلْمَجِيدُ
85:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,

85:16 فَعَّالٌ لِّمَا يُرِيدُ
85:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Atendaye ayatakayo.

85:17 هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْجُنُودِ
85:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?

85:18 فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ
85:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ya Firauni na Thamudi?

85:19 بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ فِى تَكْذِيبٍ
85:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.

85:20 وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطٌۢ
85:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

85:21 بَلْ هُوَ قُرْءَانٌ مَّجِيدٌ
85:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Bali hii ni Qur'ani tukufu

85:22 فِى لَوْحٍ مَّحْفُوظٍۭ
85:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.