Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

54 Al-Qamar ٱلْقَمَر

< Previous   55 Āyah   The Moon      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

54:1 ٱقْتَرَبَتِ ٱلسَّاعَةُ وَٱنشَقَّ ٱلْقَمَرُ
54:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!

54:2 وَإِن يَرَوْا۟ ءَايَةً يُعْرِضُوا۟ وَيَقُولُوا۟ سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ
54:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.

54:3 وَكَذَّبُوا۟ وَٱتَّبَعُوٓا۟ أَهْوَآءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ
54:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.

54:4 وَلَقَدْ جَآءَهُم مِّنَ ٱلْأَنۢبَآءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ
54:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.

54:5 حِكْمَةٌۢ بَـٰلِغَةٌ ۖ فَمَا تُغْنِ ٱلنُّذُرُ
54:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!

54:6 فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ ٱلدَّاعِ إِلَىٰ شَىْءٍ نُّكُرٍ
54:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;

54:7 خُشَّعًا أَبْصَـٰرُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌ مُّنتَشِرٌ
54:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,

54:8 مُّهْطِعِينَ إِلَى ٱلدَّاعِ ۖ يَقُولُ ٱلْكَـٰفِرُونَ هَـٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌ
54:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.

54:9 ۞ كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ فَكَذَّبُوا۟ عَبْدَنَا وَقَالُوا۟ مَجْنُونٌ وَٱزْدُجِرَ
54:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.

54:10 فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنِّى مَغْلُوبٌ فَٱنتَصِرْ
54:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!

54:11 فَفَتَحْنَآ أَبْوَٰبَ ٱلسَّمَآءِ بِمَآءٍ مُّنْهَمِرٍ
54:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.

54:12 وَفَجَّرْنَا ٱلْأَرْضَ عُيُونًا فَٱلْتَقَى ٱلْمَآءُ عَلَىٰٓ أَمْرٍ قَدْ قُدِرَ
54:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.

54:13 وَحَمَلْنَـٰهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَٰحٍ وَدُسُرٍ
54:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.

54:14 تَجْرِى بِأَعْيُنِنَا جَزَآءً لِّمَن كَانَ كُفِرَ
54:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.

54:15 وَلَقَد تَّرَكْنَـٰهَآ ءَايَةً فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
54:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?

54:16 فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
54:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.

54:17 وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
54:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?

54:18 كَذَّبَتْ عَادٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
54:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

54:19 إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًا صَرْصَرًا فِى يَوْمِ نَحْسٍ مُّسْتَمِرٍّ
54:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,

54:20 تَنزِعُ ٱلنَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ مُّنقَعِرٍ
54:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.

54:21 فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
54:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

54:22 وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
54:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?

54:23 كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ
54:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.

54:24 فَقَالُوٓا۟ أَبَشَرًا مِّنَّا وَٰحِدًا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذًا لَّفِى ضَلَـٰلٍ وَسُعُرٍ
54:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!

54:25 أَءُلْقِىَ ٱلذِّكْرُ عَلَيْهِ مِنۢ بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌ
54:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!

54:26 سَيَعْلَمُونَ غَدًا مَّنِ ٱلْكَذَّابُ ٱلْأَشِرُ
54:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.

54:27 إِنَّا مُرْسِلُوا۟ ٱلنَّاقَةِ فِتْنَةً لَّهُمْ فَٱرْتَقِبْهُمْ وَٱصْطَبِرْ
54:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.

54:28 وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ ٱلْمَآءَ قِسْمَةٌۢ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍ مُّحْتَضَرٌ
54:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.

54:29 فَنَادَوْا۟ صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ
54:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.

54:30 فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
54:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!

54:31 إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةً وَٰحِدَةً فَكَانُوا۟ كَهَشِيمِ ٱلْمُحْتَظِرِ
54:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.

54:32 وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
54:32
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?

54:33 كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍۭ بِٱلنُّذُرِ
54:33
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.

54:34 إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ ۖ نَّجَّيْنَـٰهُم بِسَحَرٍ
54:34
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.

54:35 نِّعْمَةً مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِى مَن شَكَرَ
54:35
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.

54:36 وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا۟ بِٱلنُّذُرِ
54:36
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.

54:37 وَلَقَدْ رَٰوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِۦ فَطَمَسْنَآ أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ
54:37
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!

54:38 وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌ مُّسْتَقِرٌّ
54:38
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.

54:39 فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ
54:39
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!

54:40 وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
54:40
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?

54:41 وَلَقَدْ جَآءَ ءَالَ فِرْعَوْنَ ٱلنُّذُرُ
54:41
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.

54:42 كَذَّبُوا۟ بِـَٔايَـٰتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَـٰهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ
54:42
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.

54:43 أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌ مِّنْ أُو۟لَـٰٓئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَآءَةٌ فِى ٱلزُّبُرِ
54:43
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?

54:44 أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌ مُّنتَصِرٌ
54:44
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.

54:45 سَيُهْزَمُ ٱلْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ ٱلدُّبُرَ
54:45
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.

54:46 بَلِ ٱلسَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَٱلسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ
54:46
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.

54:47 إِنَّ ٱلْمُجْرِمِينَ فِى ضَلَـٰلٍ وَسُعُرٍ
54:47
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.

54:48 يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِى ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا۟ مَسَّ سَقَرَ
54:48
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!

54:49 إِنَّا كُلَّ شَىْءٍ خَلَقْنَـٰهُ بِقَدَرٍ
54:49
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.

54:50 وَمَآ أَمْرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٌ كَلَمْحٍۭ بِٱلْبَصَرِ
54:50
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.

54:51 وَلَقَدْ أَهْلَكْنَآ أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
54:51
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?

54:52 وَكُلُّ شَىْءٍ فَعَلُوهُ فِى ٱلزُّبُرِ
54:52
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.

54:53 وَكُلُّ صَغِيرٍ وَكَبِيرٍ مُّسْتَطَرٌ
54:53
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.

54:54 إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّـٰتٍ وَنَهَرٍ
54:54
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.

54:55 فِى مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍۭ
54:55
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.