Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

51 Adh-Dhāriyāt ٱلذَّارِيَات

< Previous   60 Āyah   The Winnowing Winds      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

51:1 وَٱلذَّٰرِيَـٰتِ ذَرْوًا
51:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,

51:2 فَٱلْحَـٰمِلَـٰتِ وِقْرًا
51:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na zinazo beba mizigo,

51:3 فَٱلْجَـٰرِيَـٰتِ يُسْرًا
51:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na zinazo kwenda kwa wepesi.

51:4 فَٱلْمُقَسِّمَـٰتِ أَمْرًا
51:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na zinazo gawanya kwa amri,

51:5 إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ
51:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,

51:6 وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٌ
51:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.

51:7 وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْحُبُكِ
51:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Naapa kwa mbingu zenye njia,

51:8 إِنَّكُمْ لَفِى قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ
51:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.

51:9 يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ
51:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.

51:10 قُتِلَ ٱلْخَرَّٰصُونَ
51:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wazushi wameangamizwa.

51:11 ٱلَّذِينَ هُمْ فِى غَمْرَةٍ سَاهُونَ
51:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ambao wameghafilika katika ujinga.

51:12 يَسْـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلدِّينِ
51:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?

51:13 يَوْمَ هُمْ عَلَى ٱلنَّارِ يُفْتَنُونَ
51:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.

51:14 ذُوقُوا۟ فِتْنَتَكُمْ هَـٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تَسْتَعْجِلُونَ
51:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.

51:15 إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
51:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.

51:16 ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ
51:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.

51:17 كَانُوا۟ قَلِيلًا مِّنَ ٱلَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ
51:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.

51:18 وَبِٱلْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ
51:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.

51:19 وَفِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ
51:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.

51:20 وَفِى ٱلْأَرْضِ ءَايَـٰتٌ لِّلْمُوقِنِينَ
51:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.

51:21 وَفِىٓ أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ
51:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?

51:22 وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ
51:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.

51:23 فَوَرَبِّ ٱلسَّمَآءِ وَٱلْأَرْضِ إِنَّهُۥ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَآ أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ
51:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.

51:24 هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَٰهِيمَ ٱلْمُكْرَمِينَ
51:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?

51:25 إِذْ دَخَلُوا۟ عَلَيْهِ فَقَالُوا۟ سَلَـٰمًا ۖ قَالَ سَلَـٰمٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
51:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.

51:26 فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ
51:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.

51:27 فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
51:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?

51:28 فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا۟ لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَـٰمٍ عَلِيمٍ
51:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.

51:29 فَأَقْبَلَتِ ٱمْرَأَتُهُۥ فِى صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ
51:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!

51:30 قَالُوا۟ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْحَكِيمُ ٱلْعَلِيمُ
51:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.

51:31 ۞ قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا ٱلْمُرْسَلُونَ
51:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?

51:32 قَالُوٓا۟ إِنَّآ أُرْسِلْنَآ إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
51:32
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,

51:33 لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ
51:33
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tuwatupie mawe ya udongo,

51:34 مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ
51:34
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.

51:35 فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
51:35
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.

51:36 فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ ٱلْمُسْلِمِينَ
51:36
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!

51:37 وَتَرَكْنَا فِيهَآ ءَايَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ
51:37
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.

51:38 وَفِى مُوسَىٰٓ إِذْ أَرْسَلْنَـٰهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَـٰنٍ مُّبِينٍ
51:38
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.

51:39 فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِۦ وَقَالَ سَـٰحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
51:39
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!

51:40 فَأَخَذْنَـٰهُ وَجُنُودَهُۥ فَنَبَذْنَـٰهُمْ فِى ٱلْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ
51:40
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.

51:41 وَفِى عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ ٱلرِّيحَ ٱلْعَقِيمَ
51:41
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.

51:42 مَا تَذَرُ مِن شَىْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَٱلرَّمِيمِ
51:42
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.

51:43 وَفِى ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا۟ حَتَّىٰ حِينٍ
51:43
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.

51:44 فَعَتَوْا۟ عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّـٰعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ
51:44
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.

51:45 فَمَا ٱسْتَطَـٰعُوا۟ مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا۟ مُنتَصِرِينَ
51:45
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.

51:46 وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَوْمًا فَـٰسِقِينَ
51:46
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.

51:47 وَٱلسَّمَآءَ بَنَيْنَـٰهَا بِأَيْي۟دٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ
51:47
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.

51:48 وَٱلْأَرْضَ فَرَشْنَـٰهَا فَنِعْمَ ٱلْمَـٰهِدُونَ
51:48
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!

51:49 وَمِن كُلِّ شَىْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
51:49
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.

51:50 فَفِرُّوٓا۟ إِلَى ٱللَّهِ ۖ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
51:50
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

51:51 وَلَا تَجْعَلُوا۟ مَعَ ٱللَّهِ إِلَـٰهًا ءَاخَرَ ۖ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
51:51
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

51:52 كَذَٰلِكَ مَآ أَتَى ٱلَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا۟ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
51:52
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.

51:53 أَتَوَاصَوْا۟ بِهِۦ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ
51:53
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.

51:54 فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَآ أَنتَ بِمَلُومٍ
51:54
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.

51:55 وَذَكِّرْ فَإِنَّ ٱلذِّكْرَىٰ تَنفَعُ ٱلْمُؤْمِنِينَ
51:55
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.

51:56 وَمَا خَلَقْتُ ٱلْجِنَّ وَٱلْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ
51:56
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.

51:57 مَآ أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَآ أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ
51:57
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.

51:58 إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلرَّزَّاقُ ذُو ٱلْقُوَّةِ ٱلْمَتِينُ
51:58
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.

51:59 فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَـٰبِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ
51:59
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.

51:60 فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا۟ مِن يَوْمِهِمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ
51:60
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.