Selected
Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani
Abdullah Yusuf Ali
Abdul Majid Daryabadi
Abul Ala Maududi
Ahmed Ali
Ahmed Raza Khan
A. J. Arberry
Ali Quli Qarai
Hasan al-Fatih Qaribullah and Ahmad Darwish
Mohammad Habib Shakir
Mohammed Marmaduke William Pickthall
Muhammad Sarwar
Muhammad Taqi-ud-Din al-Hilali and Muhammad Muhsin Khan
Safi-ur-Rahman al-Mubarakpuri
Saheeh International
Talal Itani
Transliteration
Wahiduddin Khan
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.
51:1
وَٱلذَّٰرِيَـٰتِ ذَرْوًا
51:1
Naapa kwa pepo zinazo tawanya, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:2
فَٱلْحَـٰمِلَـٰتِ وِقْرًا
51:2
Na zinazo beba mizigo, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:3
فَٱلْجَـٰرِيَـٰتِ يُسْرًا
51:3
Na zinazo kwenda kwa wepesi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:4
فَٱلْمُقَسِّمَـٰتِ أَمْرًا
51:4
Na zinazo gawanya kwa amri, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:5
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ
51:5
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:6
وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٌ
51:6
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:7
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْحُبُكِ
51:7
Naapa kwa mbingu zenye njia, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:8
إِنَّكُمْ لَفِى قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ
51:8
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:9
يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ
51:9
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:10
قُتِلَ ٱلْخَرَّٰصُونَ
51:10
Wazushi wameangamizwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:11
ٱلَّذِينَ هُمْ فِى غَمْرَةٍ سَاهُونَ
51:11
Ambao wameghafilika katika ujinga. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:12
يَسْـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلدِّينِ
51:12
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:13
يَوْمَ هُمْ عَلَى ٱلنَّارِ يُفْتَنُونَ
51:13
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:14
ذُوقُوا۟ فِتْنَتَكُمْ هَـٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تَسْتَعْجِلُونَ
51:14
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:15
إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
51:15
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:16
ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ
51:16
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:17
كَانُوا۟ قَلِيلًا مِّنَ ٱلَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ
51:17
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:18
وَبِٱلْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ
51:18
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:19
وَفِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ
51:19
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:20
وَفِى ٱلْأَرْضِ ءَايَـٰتٌ لِّلْمُوقِنِينَ
51:20
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:21
وَفِىٓ أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ
51:21
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:22
وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ
51:22
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:23
فَوَرَبِّ ٱلسَّمَآءِ وَٱلْأَرْضِ إِنَّهُۥ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَآ أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ
51:23
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:24
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَٰهِيمَ ٱلْمُكْرَمِينَ
51:24
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:25
إِذْ دَخَلُوا۟ عَلَيْهِ فَقَالُوا۟ سَلَـٰمًا ۖ قَالَ سَلَـٰمٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
51:25
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:26
فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ
51:26
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:27
فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
51:27
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:28
فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا۟ لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَـٰمٍ عَلِيمٍ
51:28
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:29
فَأَقْبَلَتِ ٱمْرَأَتُهُۥ فِى صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ
51:29
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:30
قَالُوا۟ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْحَكِيمُ ٱلْعَلِيمُ
51:30
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:31
۞ قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا ٱلْمُرْسَلُونَ
51:31
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:32
قَالُوٓا۟ إِنَّآ أُرْسِلْنَآ إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
51:32
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:33
لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ
51:33
Tuwatupie mawe ya udongo, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:34
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ
51:34
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:35
فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
51:35
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:36
فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ ٱلْمُسْلِمِينَ
51:36
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:37
وَتَرَكْنَا فِيهَآ ءَايَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ
51:37
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:38
وَفِى مُوسَىٰٓ إِذْ أَرْسَلْنَـٰهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَـٰنٍ مُّبِينٍ
51:38
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:39
فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِۦ وَقَالَ سَـٰحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
51:39
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:40
فَأَخَذْنَـٰهُ وَجُنُودَهُۥ فَنَبَذْنَـٰهُمْ فِى ٱلْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ
51:40
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:41
وَفِى عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ ٱلرِّيحَ ٱلْعَقِيمَ
51:41
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:42
مَا تَذَرُ مِن شَىْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَٱلرَّمِيمِ
51:42
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:43
وَفِى ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا۟ حَتَّىٰ حِينٍ
51:43
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:44
فَعَتَوْا۟ عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّـٰعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ
51:44
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:45
فَمَا ٱسْتَطَـٰعُوا۟ مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا۟ مُنتَصِرِينَ
51:45
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:46
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَوْمًا فَـٰسِقِينَ
51:46
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:47
وَٱلسَّمَآءَ بَنَيْنَـٰهَا بِأَيْي۟دٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ
51:47
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:48
وَٱلْأَرْضَ فَرَشْنَـٰهَا فَنِعْمَ ٱلْمَـٰهِدُونَ
51:48
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:49
وَمِن كُلِّ شَىْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
51:49
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:50
فَفِرُّوٓا۟ إِلَى ٱللَّهِ ۖ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
51:50
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:51
وَلَا تَجْعَلُوا۟ مَعَ ٱللَّهِ إِلَـٰهًا ءَاخَرَ ۖ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
51:51
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:52
كَذَٰلِكَ مَآ أَتَى ٱلَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا۟ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
51:52
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:53
أَتَوَاصَوْا۟ بِهِۦ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ
51:53
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:54
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَآ أَنتَ بِمَلُومٍ
51:54
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:55
وَذَكِّرْ فَإِنَّ ٱلذِّكْرَىٰ تَنفَعُ ٱلْمُؤْمِنِينَ
51:55
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:56
وَمَا خَلَقْتُ ٱلْجِنَّ وَٱلْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ
51:56
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:57
مَآ أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَآ أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ
51:57
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:58
إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلرَّزَّاقُ ذُو ٱلْقُوَّةِ ٱلْمَتِينُ
51:58
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:59
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَـٰبِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ
51:59
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
51:60
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا۟ مِن يَوْمِهِمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ
51:60
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)