Selected
Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani
Abdullah Yusuf Ali
Abdul Majid Daryabadi
Abul Ala Maududi
Ahmed Ali
Ahmed Raza Khan
A. J. Arberry
Ali Quli Qarai
Hasan al-Fatih Qaribullah and Ahmad Darwish
Mohammad Habib Shakir
Mohammed Marmaduke William Pickthall
Muhammad Sarwar
Muhammad Taqi-ud-Din al-Hilali and Muhammad Muhsin Khan
Safi-ur-Rahman al-Mubarakpuri
Saheeh International
Talal Itani
Transliteration
Wahiduddin Khan
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.
68:1
نٓ ۚ وَٱلْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ
68:1
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:2
مَآ أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ
68:2
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:3
وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ
68:3
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:4
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ
68:4
Na hakika wewe una tabia tukufu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:5
فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ
68:5
Karibu utaona, na wao wataona, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:6
بِأَييِّكُمُ ٱلْمَفْتُونُ
68:6
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:7
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعْلَمُ بِٱلْمُهْتَدِينَ
68:7
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:8
فَلَا تُطِعِ ٱلْمُكَذِّبِينَ
68:8
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:9
وَدُّوا۟ لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ
68:9
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:10
وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ
68:10
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:11
هَمَّازٍ مَّشَّآءٍۭ بِنَمِيمٍ
68:11
Mtapitapi, apitaye akifitini, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:12
مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
68:12
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:13
عُتُلٍّۭ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
68:13
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:14
أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ
68:14
Ati kwa kuwa ana mali na watoto! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:15
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَـٰتُنَا قَالَ أَسَـٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ
68:15
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:16
سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلْخُرْطُومِ
68:16
Tutamtia kovu juu ya pua yake. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:17
إِنَّا بَلَوْنَـٰهُمْ كَمَا بَلَوْنَآ أَصْحَـٰبَ ٱلْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا۟ لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ
68:17
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:18
وَلَا يَسْتَثْنُونَ
68:18
Wala hawakusema: Mungu akipenda! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:19
فَطَافَ عَلَيْهَا طَآئِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَآئِمُونَ
68:19
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:20
فَأَصْبَحَتْ كَٱلصَّرِيمِ
68:20
Likawa kama usiku wa giza. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:21
فَتَنَادَوْا۟ مُصْبِحِينَ
68:21
Asubuhi wakaitana. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:22
أَنِ ٱغْدُوا۟ عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَـٰرِمِينَ
68:22
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:23
فَٱنطَلَقُوا۟ وَهُمْ يَتَخَـٰفَتُونَ
68:23
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:24
أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا ٱلْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ
68:24
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:25
وَغَدَوْا۟ عَلَىٰ حَرْدٍ قَـٰدِرِينَ
68:25
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:26
فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوٓا۟ إِنَّا لَضَآلُّونَ
68:26
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:27
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
68:27
Bali tumenyimwa! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:28
قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ
68:28
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:29
قَالُوا۟ سُبْحَـٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَـٰلِمِينَ
68:29
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:30
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَـٰوَمُونَ
68:30
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:31
قَالُوا۟ يَـٰوَيْلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَـٰغِينَ
68:31
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:32
عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ
68:32
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:33
كَذَٰلِكَ ٱلْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ ٱلْـَٔاخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا۟ يَعْلَمُونَ
68:33
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua! - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:34
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
68:34
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:35
أَفَنَجْعَلُ ٱلْمُسْلِمِينَ كَٱلْمُجْرِمِينَ
68:35
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:36
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
68:36
Mna nini? Mnahukumu vipi? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:37
أَمْ لَكُمْ كِتَـٰبٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ
68:37
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:38
إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
68:38
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:39
أَمْ لَكُمْ أَيْمَـٰنٌ عَلَيْنَا بَـٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ ٱلْقِيَـٰمَةِ ۙ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ
68:39
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:40
سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
68:40
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:41
أَمْ لَهُمْ شُرَكَآءُ فَلْيَأْتُوا۟ بِشُرَكَآئِهِمْ إِن كَانُوا۟ صَـٰدِقِينَ
68:41
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:42
يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ
68:42
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza, - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:43
خَـٰشِعَةً أَبْصَـٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۖ وَقَدْ كَانُوا۟ يُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمْ سَـٰلِمُونَ
68:43
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima - - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:44
فَذَرْنِى وَمَن يُكَذِّبُ بِهَـٰذَا ٱلْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ
68:44
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:45
وَأُمْلِى لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِى مَتِينٌ
68:45
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:46
أَمْ تَسْـَٔلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ
68:46
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:47
أَمْ عِندَهُمُ ٱلْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ
68:47
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika? - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:48
فَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ
68:48
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:49
لَّوْلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ
68:49
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:50
فَٱجْتَبَـٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
68:50
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:51
وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَـٰرِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا۟ ٱلذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجْنُونٌ
68:51
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)
68:52
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَـٰلَمِينَ
68:52
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote. - Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili)