Selected

Original Text
Ali Muhsin Al-Barwani

Available Translations

56 Al-Wāqi`ah ٱلْوَاقِعَة

< Previous   96 Āyah   The Inevitable      Next >  

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
In the name of Allah, Most Gracious, Most Merciful.

56:1 إِذَا وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ
56:1
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Litakapo tukia hilo Tukio

56:2 لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ
56:2
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.

56:3 خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ
56:3
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Literemshalo linyanyualo,

56:4 إِذَا رُجَّتِ ٱلْأَرْضُ رَجًّا
56:4
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,

56:5 وَبُسَّتِ ٱلْجِبَالُ بَسًّا
56:5
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na milima itapo sagwasagwa,

56:6 فَكَانَتْ هَبَآءً مُّنۢبَثًّا
56:6
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,

56:7 وَكُنتُمْ أَزْوَٰجًا ثَلَـٰثَةً
56:7
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-

56:8 فَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ
56:8
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

56:9 وَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ
56:9
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

56:10 وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ
56:10
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wa mbele watakuwa mbele.

56:11 أُو۟لَـٰٓئِكَ ٱلْمُقَرَّبُونَ
56:11
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hao ndio watakao karibishwa

56:12 فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
56:12
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika Bustani zenye neema.

56:13 ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
56:13
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Fungu kubwa katika wa mwanzo,

56:14 وَقَلِيلٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ
56:14
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wachache katika wa mwisho.

56:15 عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ
56:15
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.

56:16 مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيْهَا مُتَقَـٰبِلِينَ
56:16
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakiviegemea wakielekeana.

56:17 يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌ مُّخَلَّدُونَ
56:17
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,

56:18 بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ
56:18
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.

56:19 لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ
56:19
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

56:20 وَفَـٰكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
56:20
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na matunda wayapendayo,

56:21 وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ
56:21
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.

56:22 وَحُورٌ عِينٌ
56:22
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Mahurulaini,

56:23 كَأَمْثَـٰلِ ٱللُّؤْلُؤِ ٱلْمَكْنُونِ
56:23
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.

56:24 جَزَآءًۢ بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ
56:24
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

56:25 لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا
56:25
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,

56:26 إِلَّا قِيلًا سَلَـٰمًا سَلَـٰمًا
56:26
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.

56:27 وَأَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ
56:27
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

56:28 فِى سِدْرٍ مَّخْضُودٍ
56:28
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika mikunazi isiyo na miba,

56:29 وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ
56:29
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na migomba iliyo pangiliwa,

56:30 وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ
56:30
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kivuli kilicho tanda,

56:31 وَمَآءٍ مَّسْكُوبٍ
56:31
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na maji yanayo miminika,

56:32 وَفَـٰكِهَةٍ كَثِيرَةٍ
56:32
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na matunda mengi,

56:33 لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ
56:33
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hayatindikii wala hayakatazwi,

56:34 وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ
56:34
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.

56:35 إِنَّآ أَنشَأْنَـٰهُنَّ إِنشَآءً
56:35
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,

56:36 فَجَعَلْنَـٰهُنَّ أَبْكَارًا
56:36
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na tutawafanya vijana,

56:37 عُرُبًا أَتْرَابًا
56:37
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

56:38 لِّأَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ
56:38
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa ajili ya watu wa kuliani.

56:39 ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
56:39
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Fungu kubwa katika wa mwanzo,

56:40 وَثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ
56:40
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na fungu kubwa katika wa mwisho.

56:41 وَأَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ
56:41
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

56:42 فِى سَمُومٍ وَحَمِيمٍ
56:42
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,

56:43 وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ
56:43
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kivuli cha moshi mweusi,

56:44 لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ
56:44
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.

56:45 إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ
56:45
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

56:46 وَكَانُوا۟ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلْحِنثِ ٱلْعَظِيمِ
56:46
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,

56:47 وَكَانُوا۟ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
56:47
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?

56:48 أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ
56:48
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Au baba zetu wa zamani?

56:49 قُلْ إِنَّ ٱلْأَوَّلِينَ وَٱلْـَٔاخِرِينَ
56:49
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho

56:50 لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَـٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
56:50
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

56:51 ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلْمُكَذِّبُونَ
56:51
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,

56:52 لَـَٔاكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ
56:52
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

56:53 فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ
56:53
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

56:54 فَشَـٰرِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ ٱلْحَمِيمِ
56:54
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.

56:55 فَشَـٰرِبُونَ شُرْبَ ٱلْهِيمِ
56:55
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.

56:56 هَـٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ ٱلدِّينِ
56:56
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.

56:57 نَحْنُ خَلَقْنَـٰكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ
56:57
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

56:58 أَفَرَءَيْتُم مَّا تُمْنُونَ
56:58
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?

56:59 ءَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلْخَـٰلِقُونَ
56:59
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

56:60 نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ ٱلْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
56:60
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi

56:61 عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَـٰلَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِى مَا لَا تَعْلَمُونَ
56:61
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.

56:62 وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ ٱلنَّشْأَةَ ٱلْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ
56:62
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

56:63 أَفَرَءَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ
56:63
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?

56:64 ءَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُۥٓ أَمْ نَحْنُ ٱلزَّٰرِعُونَ
56:64
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

56:65 لَوْ نَشَآءُ لَجَعَلْنَـٰهُ حُطَـٰمًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ
56:65
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,

56:66 إِنَّا لَمُغْرَمُونَ
56:66
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;

56:67 بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
56:67
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Bali sisi tumenyimwa.

56:68 أَفَرَءَيْتُمُ ٱلْمَآءَ ٱلَّذِى تَشْرَبُونَ
56:68
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?

56:69 ءَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ ٱلْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنزِلُونَ
56:69
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

56:70 لَوْ نَشَآءُ جَعَلْنَـٰهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ
56:70
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

56:71 أَفَرَءَيْتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِى تُورُونَ
56:71
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Je! Mnauona moto mnao uwasha?

56:72 ءَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَآ أَمْ نَحْنُ ٱلْمُنشِـُٔونَ
56:72
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

56:73 نَحْنُ جَعَلْنَـٰهَا تَذْكِرَةً وَمَتَـٰعًا لِّلْمُقْوِينَ
56:73
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

56:74 فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ
56:74
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

56:75 ۞ فَلَآ أُقْسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ
56:75
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,

56:76 وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ
56:76
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!

56:77 إِنَّهُۥ لَقُرْءَانٌ كَرِيمٌ
56:77
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,

56:78 فِى كِتَـٰبٍ مَّكْنُونٍ
56:78
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.

56:79 لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلْمُطَهَّرُونَ
56:79
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hapana akigusaye ila walio takaswa.

56:80 تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
56:80
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

56:81 أَفَبِهَـٰذَا ٱلْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ
56:81
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

56:82 وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ
56:82
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

56:83 فَلَوْلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلْحُلْقُومَ
56:83
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,

56:84 وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ
56:84
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na nyinyi wakati huo mnatazama!

56:85 وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَـٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ
56:85
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.

56:86 فَلَوْلَآ إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ
56:86
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,

56:87 تَرْجِعُونَهَآ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ
56:87
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

56:88 فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ
56:88
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,

56:89 فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ
56:89
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

56:90 وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنْ أَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ
56:90
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,

56:91 فَسَلَـٰمٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ
56:91
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.

56:92 وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلْمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ
56:92
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,

56:93 فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ
56:93
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,

56:94 وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ
56:94
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Na kutiwa Motoni.

56:95 إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلْيَقِينِ
56:95
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

56:96 فَسَبِّحْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلْعَظِيمِ
56:96
Ali Muhsin Al-Barwani (Swahili) :
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.